You are here: Home NEWS Local News

Local News

News

YANGA YAANZA KUJIFUA

Mara baada ya kuwasili salama jana jioni katika hoteli ya Sueno Beach Side eneo la Manavgat pembeni kidogo ya jiji la Antalya kikosi cha Young Africans leo asubuhi kimeanza mazoezi ya kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu pamoja na mashindano ya kimataifa barani Afrika.

Timu ilipokelewa na wenyeji majira ya saa 11:00 jioni kwa saa za huku ikiwa ni sawa na saaa 12 kwa saa za Afrika Mashariki na moja kwa moja kikosi kilielekea katika mji wa Manavgat ambapo ndipo ilipo hoteli ya Sueno Beach Side ambapo msafara mzima umefikia.

Sueno Hotel Beach Side ni hoteli kubwa yenye hadhi ya nyota tano, ambayo ina jumla ya vyumba 760, mabwawa ya kuogelea,viwanja viwili vya mpira vya mazoezi kimoja kikiwa na nyasi za kawaida na kingine nyasi za bandia.

Kocha msaidizi wa Young Africans Charles Boniface Mkwasa amesema anashukuru kikosi chake kimefika salama na wachezaji wote wakiwa katika hali nzuri kiafya na kifikra hivyo anatarajiwa mazoezi yatakayoanza leo yatasaidia kuiweka timu katika hali nzuri na kuwa tayari kwa mashindano.

"Kazi yangu kubwa ni kukiandaa kikosi kiwe katika hali nzuri ili pindi tutakaporejea nchini timu iwe fiti na tayari kwa ajili ya mashindano, kwa hali ilivyo nzuri na mazingira naamini timu itabadilika na kurejea nchini ikiwa katika kiwango cha kizuri cha ushindani" alisema Mkwasa

Young Africans inatarajia kucheza mchezo wake wa kwanza wa kirafiki dhidi ya timu ya Ankara Sekerspor iliyopo Ligi Daraja la Kwanza nchini Uturuki.

Aidha timu ya Sivasspor iliyopo Ligi Kuu nchini Uturuki inayonolewa na mchezaji wa zamani Real Madrid na timu ya Taifa ya Brazil Roberto Carlos pia imeweka kambi katika hoteli ya Sueno na leo asubuhi kabla ya Young Africans kuanza mazoezi waliweza kupiga picha ya pamoja na gwiji huyo.

 

News

YANGA YAANZA KUJIFUA

VIEWED 1465 TIMES

Mara baada ya kuwasili salama jana jioni katika hoteli ya Sueno Beach Side eneo la Manavgat pembeni kidogo ya jiji la Antalya kikosi cha Young Africans leo asubuhi kimeanza mazoezi ya kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu pamoja na mashindano ya kimataifa barani Afrika.

Last Updated on Friday, 10 January 2014 16:28

Read more...

 

News

YANGA HIYOOO UTURUKI

VIEWED 3718 TIMES

Msafara wa watu 33 wakiwemo wachezaji 27 unatarajia kuondoka usiku wa leo kuelekea nchini Uturuki kwa shirika la ndege la Uturki (Turkish Airlines) kuweka kambi ya mafunzo kwa muda wa takribani wiki mbili kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom pamoja na mashindano ya kimataifa.

Last Updated on Wednesday, 08 January 2014 19:42

Read more...

   

News

YANGA YAANZA KUJIFUA

VIEWED 2777 TIMES

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara timu ya Young Africans leo imeeanza kujifua katika viwanja vya bora Mabatini Kijitonyama kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu na mashindano ya kimataifa chini ya kocha msaidizi Charles Boniface Mkwasa.

Last Updated on Friday, 03 January 2014 16:53

Read more...

 

News

MKWASA, PONDAMALI, KUINOA YANGA

VIEWED 3075 TIMES

Uongozi wa Young Africans SC umepata warithi wa nafasi tatu za benchi la ufundi (Charles Boniface Mkwasa, Juma Pondamali na Dr. Suphian Juma), huku wakiendelea na mchakato kumpata kocha mkuu ambaye atachukua nafasi ya mholanzi Ernie Brandts aliyesitishiwa mkataba wake mwishoni mwa mwaka 2013.

Last Updated on Thursday, 02 January 2014 17:55

Read more...

   

Facebook Twitter YouTube
  • FACEBOOK

  • TWITTER

mod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_counter
mod_vvisit_counterToday1267
mod_vvisit_counterYesterday11260
mod_vvisit_counterThis week20256
mod_vvisit_counterLast week35641
mod_vvisit_counterThis month75846
mod_vvisit_counterLast month188334
mod_vvisit_counterAll days1464569

We have: 69 guests, 6 bots online
Your IP: 207.241.237.229
Mozilla 5.0, 
Today: Feb 14, 2014