You are here: Home NEWS Local News OKWI AWASILI RASMI YANGA

OKWI AWASILI RASMI YANGA

E-mail Print PDF
VIEWED 4586 TIMES
Mshambuliaji wa kimataifa kutoka nchini Uganda Emmanuel Okwi amewasili leo mchana majira ya saa 9:45 katika uwanja wa ndege wa Mwalimu JK Nyererer akitokea nchini Uganda kwa shirika la ndege la Rwanda Air.

Okwi amekuja kujiunga na timu yake mpya Yanga SC ambayo ataanza kuitumikia katika mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom na mashindano ya Kimataifa.
Mara baada ya kuwasili JK Nyerere Okwi alipokelewa na vipngozi wa kamati ya mashindano sambamba na washabiki, wapenzi na wadau wa soka kwa ujumla.
Okwi akiongea na waandishi wa habari uwanja wa ndege amesema anashukuru kwa kufika salama jijini Dar es Salaam na hasa katika timu yake mpya ya Yanga.
Kikubwa ameahidi kucheza kwa uwezo wake wote kuhakikisha anaisaidia timu yake mpya kufanya vizuri katika mashindano yote.
Okwi mara baada ya kuwasalimia washabiki na wanachama wa Yanga uwanja wa Kaunda moja kwa moja ameungana na wachezaji wenzake katika kambi iliyopo Protea kujiandaa na mchezo wa jumapili.
Last Updated ( Thursday, 19 December 2013 17:50 )  

Facebook Twitter YouTube
  • FACEBOOK

  • TWITTER

mod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_counter
mod_vvisit_counterToday4356
mod_vvisit_counterYesterday5042
mod_vvisit_counterThis week14063
mod_vvisit_counterLast week35757
mod_vvisit_counterThis month149215
mod_vvisit_counterLast month188334
mod_vvisit_counterAll days1537938

We have: 58 guests, 3 bots online
Your IP: 204.236.235.245
 , 
Today: Feb 26, 2014