You are here: Home NEWS Local News YANGA KUIVAA SC VILLA KESHO

YANGA KUIVAA SC VILLA KESHO

E-mail Print PDF

VIEWED 813 TIMES

Young Africans kesho itashuka dimba la uwanja wa Taifa kucheza mchezo wa kirafiki wa kimataifa na timu ya Sports Club Villa kutoka nchini Uganda, mchezo utakaoanza majira ya saa 10:00 jioni kwa saa za Afrika Mashariki.

Kikosi cha Young Africans kitautumia mchezo huo wa kirafiki wa kimataifa kwa ajili ya kujiaanda na msimu mpya wa Ligi Kuu nchini na pia itakua ni sehemu ya maandalizi mchezo wa ngao ya Hisani dhidi ya Azam FC jumamosi Agosti 17,2013.

Kocha mkuu wa Yanga Ernie Brandts mara baada ya mazoezi ya leo amesema anashukuru kikosi chake chote kimekamilika na kwa sasa hakuna mchezaji hata mmoja majeruhi hali inayompa nafasi nzuri ya kumtumia mchezaji yoyote katika michezo watakayocheza.

'Mchezo wa kesho dhidi ya Sports Club Villa ya nchini Uganda utakua ni kipimo kizuri kwetu kesho, kwani utakua ni mchezo wa mwisho kabla ya kuanza kwa mikikimikiki ya Ligi Kuu ya Vodacom na kucheza mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Azam FC' alisema Brandts.

Viingilio vya mchezo huo dhidi ya SC Villa ni:

VIP A Tshs 20,000/=

VIP B Tshs 15,000/=

VIP C Tshs 10,000/=

Orange, Blue & Green Tshs 5,000/=

Wapenzi wa soka na washabiki wa klabu ya Yanga wanaombwa kujitokeza kwa wingi kesho kuja kuiona timu ya Yanga ambayo imekamilika kuelekea kwenye kinyang'anyiro cha kutwaa Ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom msimu wa 2013/2014

 

 

Last Updated ( Saturday, 10 August 2013 11:55 )  

Facebook Twitter YouTube
  • FACEBOOK

  • TWITTER

mod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_counter
mod_vvisit_counterToday1966
mod_vvisit_counterYesterday3099
mod_vvisit_counterThis week5065
mod_vvisit_counterLast week19629
mod_vvisit_counterThis month20927
mod_vvisit_counterLast month76582
mod_vvisit_counterAll days887394

We have: 18 guests online
Your IP: 207.241.237.231
Mozilla 5.0, 
Today: Oct 08, 2013