You are here: Home NEWS Local News YANGA UTAIPENDA TU, YAICHAPA OLJORO 3-0

YANGA UTAIPENDA TU, YAICHAPA OLJORO 3-0

E-mail Print PDF
VIEWED 1734 TIMES
"sita, saba, nane,tisa, kumi , kumi na sita, kumi na nane, ishirini na tano, ishirini na sita"
Hivyo ndivyo washabiki, wapenzi na wanachama wa klabu ya Young Africans Sports Club leo walivyokua wakihesabu pasi murua (sambusa) wakati mchezo ukiendelea huku wakicheza na kufurahi kwa makofi, ambapo timu ya Yanga ilikua inaongoza kwa mabao 3-0, katika mchezo uliomalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhid ya timu ya JKT Oljoro mchezo uliofanyika katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Young Africans imeendelea kujiweka katika nafasi nzuri ya msimamo wa Ligi Kuu ya Vodacom baada kufikisha point 52 na mabao 40 ya kufunga, pointi 6 mbele ya timu inayoshika nafasi ya pili Azam Fc yenye pointi 46 huku timu zote zikiwa na michezo sawa 22.

Kikosi cha mholanzi Ernest Brandts kiliuanza mchezo kwa kasi na katika dakika ya 5 ya mchzo kupitia kwa mlinzi wa kati Nadir Haroub 'Cannavaro' aliipatia bao la kwanza kwa kichwa baada ya kumalizia mpira wa kona iliyokuw aimepigwa na kiungo Haruna Niyonzima.
Watoto wa jangwani walionyesha kuwa wamedhamiria kupata ushindi mnono leo kwani waliweza kucheza soka safi na la kuvutia huku Hamis Kiiza na Didier Kavumbagu wakikosa mabao ya wazi ndani ya dakika 15 za kwanza.
Kiungo chipukizi mwenye kasi Saimon Msuva aliipatia Young Africans bao pili dakika ya 19 ya mchezo kufuatia kuwazidi ujanja walinzi wa timu ya JKT Olljoro na Msuva kumchambua kwa umaridadi mlinda mlango wa JKT Oljoro na kuhesabu bao la pili kwa timu ya Yanga.
Yanga iliendelea kulishambulia lango la JKT Oljoro muda wote wa mchezo na mashuti ya washambuliaji wa Yanga yalimfanya mlinda mlnago huyo kutibiwa mara kwa mara kwa kukoa michomo ya washambuliaji wa Yanga.
Dakka ya 43, mshambuliaji wa kimataifa kutoka nchini Uganda Hamis Kiiza aliipatia Yanga bao la tatu kufuatia mpira aliopenyezewa na kiungo Frank Domayo na Kiiza kuwatoka walinzi wa JKT Oljoro na kuiandikia Yanga bao la tatu.
Mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza, Young Africans 3 - 0 JKT Oljoro.
Kipindi cha pili kilianza kwa Yanga kufanya mabadiliko ambapo waliingia Nizar Khalfani na Said Bahanuzi kuchukua nafasi za Didier Kavumbagu aliyeumia na Simon Msuva mabadiliko yaliongeza ufundi zaidi na kuutalawa mchezo kwa kipidndi chote.
Said Bahanuzi alifanyiwa madhambi wakati akiwa ndani ya eneo la hatari akijandaa kumchambua mlinda mlango wa JKT Oljoro lakini mwamuzi wa mchezo na mwamuzi wa pembeni wake hawakujali na kuendelea na mchezo.
Zikiwa zimebakia dakika tano kabla yakumalizika kwa mchezo, kiungo mshambuliaji Nizar Khalfani alikosa bao la wazi kufuatia shuti lake kuokolewa na mlinda mlango wake ambapo mpira huo ulipigwa kona ambayo haikuzaa matunda.
Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika, Young Africans 3 - 0 JKT Oljoro.

Kocha mkuu wa Yanga Ernest Brandts amesema anashukuru timu yake kupata kwa ushindi katika mchezo wa leo, kipindi cha kwanza timu yangu ilicheza kwa nguvu na kupata mabao ya mapema hali iliyoplekea kipindi cha pili kucheza soka la burudani.
Timu imekua na mabadiliko makubwa sana kiuchezaji na leo timu imecheza soka safi la burudani lililoambatana na ushindi, hii ni zawadi kwa washabiki, wapenzi wa soka na wanachama wa klabu ya Yanga kuwa njia ya kutwaa ubingwa kwa sasa ni nyeupe.
Yanga inajiandaa na mchezo dhidi ya timu ya Mgambo Shooting siku ya jumatano mjini Tanga ambapo timu itasafiri siku ya jumatatu tayari kwa ajili ya mchezo huo ambao ni muhimu kwa Yanga ili kuendelea kujiweka vizuri katika nafasi ya kutwaa Ubingwa kabla ya kumalizika kwa msimu.

Young Africans: 1.Ally Mustapha 'Barthez', 2.Juma Abdul/Shadrack Nsajigwa, 3.David Luhende, 4.Nadir Haroub'Cannavaro', 5.Kelvin Yondani , 6.Athuman Idd 'Chuji', 7.Saimon Msuva/Nizar Khalfani, 8.Frank Domayo, 9.Didier Kavumbagu/Said Bahanuzi,10.Hamis Kiiza, 11.Haruna Niyonzima
Last Updated ( Saturday, 13 April 2013 20:04 )  

  • FACEBOOK PAGE

  • TWITTER FEEDS

yanga1935: I posted 5 photos on Facebook in the album "CHAMP24NS" http://t.co/jw1L47m1kO
yanga1935: Sherehe za kukabidhiwa Ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom msimu wa 2012/2013 kwa Mabingwa wapya Young Africans... http://t.co/S8GiejZjr7
yanga1935: Mpira umemalizika, Young Africans 2 - 0 Simba SC Kavumbagu ddk 4 Kiiza dkk 63
yanga1935: Dakika ya 89, Mpira umesimama kidogo, baada ya Nassoro Chollo kumsukuma Kavumbagu na wakati mwamuzi anamuulia kadondoka chini mwenyewe.
yanga1935: Dakika ya 85, anaingia Juma Abdul kuchukua nafasi ya Mbuyu Twite
yanga1935: Dakika ya 75, Young Africans 2 - 0 Simba SC Anaingia Nizar Khalfani kuchukua nafasi ya Hamis Kiiza
yanga1935: Dakika ya 75, Young Africans 1 - 0 Simba SC Anaingia Nizar Khalfani kuchukua nafasi ya Hamis Kiiza
yanga1935: Dakika ya 63, Hamis Kiiza anaipatia Young Africans bao la pili Young Africans 2 - Simba SC
yanga1935: Dakika ya 60, Young Africans 1 - 0 Simba SC
yanga1935: Kipindi cha pili cha mchezo kimeanza, Young Africans 1 - 0 Simba SC
yanga1935: KUMRADHI: bao la Yanga limefungwa na Didier Kavumbagu na sio Hamis Kiiza kama nilivyoandika awali
yanga1935: Mpira ni mapumziko, Young Africans 1 - 0 Simba SC
yanga1935: Dakika ya 30, Young Africans 1 - 0 Simba SC
yanga1935: Dakika ya 28 Simba walipata penati, akapiga Mussa Mudde na kukosa
yanga1935: Dakika ya 15, Young Africans 1 - 0 Simba SC
yanga1935: Dakika ya 4, Hamis Kiiza anaipatia Young Africans bao la kwanza
yanga1935: Mpira ndo umeanza hapa Uwanja wa Taifa kati ya wenyeji Simba SC Vs Young Africans
yanga1935: Heres Young Africans line-up to face Simba SC today: 1.Ally Mustapha - 1 2.Mbuyu Twite - 6 3.David Luhende - 29... http://t.co/XRMv18Y3vR
yanga1935: Vodacom Premier Leagu 2012/2013 Simba SC Vs Young Africans Kick-off 16:00hrs Venue: National Stadium #Tukutane... http://t.co/gD7xNq3rFs
yanga1935: Kikosi cha Mabingwa wapya wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara timu ya Young Africans leo kimefanya mazoezi yake... http://t.co/V6JQZYaJud
yanga1935: @ProsperMasau tiketi zitaanzwa kuuza kesho steers posta, u/taifa, buguruni shelly, sinza madukani, benjamin mkapa secondary, darlive
yanga1935: Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara inatarajia kufikia ukingoni siku ya jumamosi kwa kuchezwa michezo 7 katika... http://t.co/1q5ABNzjjj
yanga1935: Kikosi cha Young Africans leo kimeendelea na mazoezi katika Uwanja wa Gombani kujiandaa na mchezo wake wa mwisho... http://t.co/xF73xqFibQ
yanga1935: Somewhere in Pemba Island http://t.co/Q8sX0Dgxx7
yanga1935: Young Africans Players in Camp at Pemba Island @Yanga1935 http://t.co/LfnUq2WFth
mod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_counter
mod_vvisit_counterToday1043
mod_vvisit_counterYesterday4599
mod_vvisit_counterThis week16563
mod_vvisit_counterLast week14708
mod_vvisit_counterThis month39348
mod_vvisit_counterLast month60138
mod_vvisit_counterAll days528378

We have: 49 guests, 3 bots online
Your IP: 204.236.235.245
 , 
Today: May 19, 2013