You are here: Home NEWS Local News YANGA KUIVAA ARMINIA BIELEFELD JUMAMOSI

YANGA KUIVAA ARMINIA BIELEFELD JUMAMOSI

E-mail Print PDF
VIEWED 1382 TIMES
Timu ya Young Africans Sports Club yenye makao makuu yake jijini Dar es salaam nchini Tanzania siku ya jumamosi itashuka dimbani kucheza mchezo wa kirafiki na timu ya Arminia Bielefeld ya kutoka nchini Ujerumani, mchezo utakaofanyika katika mji wa Antalya.

Young Africans ambayo imeweka kambi ya mafunzo jijini Antalya itatumia mchezo huo kama fursa pekee ya kuweza kujipima uwezo dhidi ya timu hiyo ya Ujerumani ambayo pia imekuja kambi y amafunzo kujiandaa na mzunguko wa ligi daraja la pili nchini Ujerumani.

Kocha Mkuu wa Young Africans Ernest Brandts amesema kwao ni furaha kwa kupata nafasi ya kucheza na timu kubwa kama ya Armini Bielefeld ambayo inawachezaji wa kiwango cha kimataifa hivyo anaamini utakua ni mchezo safi na kuwavutia.

Unajua tuna siku tano (5) tangu tufike hapa mjini Antalya Uturuki na tumeshafanya mazoezi kwa siku nne (4) hivyo fursa ya kupata mchezo wa kirafiki ni nzuri sana kwetu kwani itanipa nafasi ya kuona wachezaji wangu wameshayashika kwa kiasi gani mafunzo yangu alisema 'Brandts'

Arminia Bielefeld imeshawasili mjini Antalya kwa ajili ya kambi yake ya mafunzo na hivyo kwao pia ni fursa nzuri ya kuweza kujipima uwezo na timu ya Young Africans ambao ni mabingwa mara 23 katika ligi kuu ya Tanzania.

Leo asubuhi Young Africans imeendelea na mazoezi katika viwanja wa Fame Residecne tayari kabisa kujiandaa na mchezo huo utakaochezwa siku ya jumamosi mjini Antalya.

Kikosi cha wachezaji 27 waliopo mjini Antalya wote wako katika hali nzuri na hakuna maheruhi hata mmoja hali itakayompa kocha Brandts kuamua kumtumia mchezaji yoyote katika mchezo huo.
Aidha kuhusu hali ya hewa leo jua linawaka toka asubuhi mpaka hivi sasa na kwa leo ni sentigred 23 mpaka 25, hivyo hali ya hewa ni nzuri kabis ana jua linawaka.
Last Updated ( Friday, 04 January 2013 22:37 )  
  • FACEBOOK PAGE

  • TWITTER FEEDS

yanga1935: Yanga yafanya mkutano mkuu wa wanachama salama, ajenda zote zapitishwa http://t.co/lotRChsL
yanga1935: Yanga yaichapa Black Leopard mabao 3-2 http://t.co/8XbabdSs
yanga1935: Mpira umemalizika, Young Africans 3 - 2 Black Leopard Tegete dkk 32,73, Domayo 63 Khoza dkk 47, Rodney dkk 89
yanga1935: Dakika ya 89, Rodney Ramagalela anaipatia Black Leopard bao la pili kwa mkwaju wa penati
yanga1935: Dakika ya 84, Young Africans inafanya mabadiliko anaingia George Banda anatoka Jerson Tegete
yanga1935: Dakika ya 75, Young Africans 3 - 1 Black Leopard anaingia Said Bahanuzi anatoka Didier Kavumbagu
yanga1935: Dakika ya 73, Jerson Tegete anaipatia Young Africans bao la tatu Young Africans 3 - 1 Black Leopard
yanga1935: Dakika ya 63, Frank Domayo anaipatia Young Africans bao la pili Young Africans 2 - 1 Black Leopard
yanga1935: Dakika ya 60, Young Africans 1 - 1 Black Leopard
yanga1935: Dakika ya 47, Humphrey Khoza anaipatia Black Leopard bao la kusawazisha#Young Africans 1 - 1 Black Leopard
yanga1935: wanaingia Said Mohamed, Saimon Msuva na Juma Abdul Wanatoka Kabange Twite, Mbuyu Twite na Ally Mustafa
yanga1935: Kipindi cha pili cha mchezo kimeanza, Young Africans inafanya mabadiliko wanaingia Said Mohamed, Saimon Msuva na Juma Abdul
yanga1935: Mpira ni mapumziko, Young Africans 1 - 0 Black Leopard Tegete dkk 32
yanga1935: Dakika ya 32, Jerson Tegete anaipatia Young Africans bao la kwanza kwa mkwaju wa penati
yanga1935: Dakika ya 30, Young Africans 0 - 0 Black Leopard
yanga1935: Dakika ya 15, Young Africans 0 - 0 Black Leopard
yanga1935: Mpira ndio umeanza hapa Uwanja wa Taifa kati ya Young Africans Vs Black Leopard
yanga1935: Here's Young Africans line-up to face Black Leopard today#Mustafa,Mbuyu,Oscar,Nadir,Yondani,Chuji,Kabange,Domayo,Didier,Tegete,Niyonzima
yanga1935: International Friendly Match today: #Young Africans Vs Black Leopard Kick-off 16:00hrs Venue: National Stadium
yanga1935: Yanga Vs Black Leopard kesho Taifa http://t.co/o9Uu695M
yanga1935: Yanga yaanza mazoezi baada kurejea kutoka nchini Uturuki http://t.co/WjuE9731
yanga1935: Young Africans kuivaa Black Leopard ya Afrika Kusini http://t.co/O5qJvtLG
yanga1935: Yanga yawasili Dar salama http://t.co/F8W53VAa
mod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_counter
mod_vvisit_counterToday692
mod_vvisit_counterYesterday2888
mod_vvisit_counterThis week692
mod_vvisit_counterLast week17151
mod_vvisit_counterThis month55018
mod_vvisit_counterLast month36036
mod_vvisit_counterAll days293250

We have: 34 guests, 1 members, 2 bots online
Your IP: 207.241.237.238
Mozilla 5.0, 
Today: Jan 21, 2013