You are here: Home NEWS Local News YANGA YAENDELEA KUJIFUA

YANGA YAENDELEA KUJIFUA

E-mail Print PDF
VIEWED 1131 TIMES
Kikosi cha Young Africans Sports Club kimeendelea na mazoezi yake leo katika uwanja wa Fame Residece Football uliopo Antalya kisha jioni timu ikaenda kufanya mazoezi katika ufukwe wa bahari, eneo lililopo nyuma ya hoteli Fame Residence ikiwa ni siku ya tatu katika ziara ya mafunzo nchini Uturuki kujiandaa na mzunguko wa pili wa ligi kuu ya Vodacom.
Kocha Mkuu wa klabu ya Yanga mholanzi Ernie Brandts amesema anafurahishwa na maendeleo ya kambi, kwani toka wameanza mazoezi jumatatu leo ni siku ya tatu wakiwa nchini Uturuki na anaona mabadiliko makubwa kwa wachezaji wake, huku akisema hofu iliyokuwepo kwa watanzania juu ya hali hewa ya baridi kali si kweli kwani hali ya hewa katika mjii huu ni baridi kiasi tu na hata leo katika mazoezi ya asubuhi palikuwa na jua.

Wachezaji wanaendelea kuzoea mazingira, na kujifunza mambo mengi yanayohusu soka kwani wageni mbalimbali waliofika katika mji huu wamekuwa wakipenda kujua mengi kuhusiana na timu ya Young Africans na soka la Tanzania kwa ujumla.
Majira ya saa 10 kamili jioni kwa saa za Afrika Mashariki timu ilifanya mazoezi ya ufukweni katika ufukwle wa Hotelu ya Fame Residence pemebezoni mwa Bahari ya Mediteranian.

Kocha wa makipa wa timu ya Bayern Leverkusen Detier Gansi jioni alishuhudia Young Africans ikifanya mazoezi ya ufukweni ambapo alisema amefurahia kuifahamu timu ya Yanga na wachezaji wake wanaonekana kuwa na morali ya kucheza soka, hivyo anaamin ziara hii itaisaidia timu kuwa pamoja na kujiandaa vyema na ligi alisema
Wakati huo huo mchezaji wa kimataifa wa timu ya Taifa ya Rwanda Haruna Niyonzima amewasili jioni hii kuungana na wenzake kufuatia kuchelewa kuunganisha ndege siku ya jumamosi usiku akitokea nchini Rwanda alipokuwa amekwenda kuchezea timu yake ya Taifa.
Last Updated ( Wednesday, 02 January 2013 22:05 )  
  • FACEBOOK PAGE

  • TWITTER FEEDS

yanga1935: Yanga yafanya mkutano mkuu wa wanachama salama, ajenda zote zapitishwa http://t.co/lotRChsL
yanga1935: Yanga yaichapa Black Leopard mabao 3-2 http://t.co/8XbabdSs
yanga1935: Mpira umemalizika, Young Africans 3 - 2 Black Leopard Tegete dkk 32,73, Domayo 63 Khoza dkk 47, Rodney dkk 89
yanga1935: Dakika ya 89, Rodney Ramagalela anaipatia Black Leopard bao la pili kwa mkwaju wa penati
yanga1935: Dakika ya 84, Young Africans inafanya mabadiliko anaingia George Banda anatoka Jerson Tegete
yanga1935: Dakika ya 75, Young Africans 3 - 1 Black Leopard anaingia Said Bahanuzi anatoka Didier Kavumbagu
yanga1935: Dakika ya 73, Jerson Tegete anaipatia Young Africans bao la tatu Young Africans 3 - 1 Black Leopard
yanga1935: Dakika ya 63, Frank Domayo anaipatia Young Africans bao la pili Young Africans 2 - 1 Black Leopard
yanga1935: Dakika ya 60, Young Africans 1 - 1 Black Leopard
yanga1935: Dakika ya 47, Humphrey Khoza anaipatia Black Leopard bao la kusawazisha#Young Africans 1 - 1 Black Leopard
yanga1935: wanaingia Said Mohamed, Saimon Msuva na Juma Abdul Wanatoka Kabange Twite, Mbuyu Twite na Ally Mustafa
yanga1935: Kipindi cha pili cha mchezo kimeanza, Young Africans inafanya mabadiliko wanaingia Said Mohamed, Saimon Msuva na Juma Abdul
yanga1935: Mpira ni mapumziko, Young Africans 1 - 0 Black Leopard Tegete dkk 32
yanga1935: Dakika ya 32, Jerson Tegete anaipatia Young Africans bao la kwanza kwa mkwaju wa penati
yanga1935: Dakika ya 30, Young Africans 0 - 0 Black Leopard
yanga1935: Dakika ya 15, Young Africans 0 - 0 Black Leopard
yanga1935: Mpira ndio umeanza hapa Uwanja wa Taifa kati ya Young Africans Vs Black Leopard
yanga1935: Here's Young Africans line-up to face Black Leopard today#Mustafa,Mbuyu,Oscar,Nadir,Yondani,Chuji,Kabange,Domayo,Didier,Tegete,Niyonzima
yanga1935: International Friendly Match today: #Young Africans Vs Black Leopard Kick-off 16:00hrs Venue: National Stadium
yanga1935: Yanga Vs Black Leopard kesho Taifa http://t.co/o9Uu695M
yanga1935: Yanga yaanza mazoezi baada kurejea kutoka nchini Uturuki http://t.co/WjuE9731
yanga1935: Young Africans kuivaa Black Leopard ya Afrika Kusini http://t.co/O5qJvtLG
yanga1935: Yanga yawasili Dar salama http://t.co/F8W53VAa
mod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_counter
mod_vvisit_counterToday692
mod_vvisit_counterYesterday2888
mod_vvisit_counterThis week692
mod_vvisit_counterLast week17151
mod_vvisit_counterThis month55018
mod_vvisit_counterLast month36036
mod_vvisit_counterAll days293250

We have: 34 guests, 1 members, 2 bots online
Your IP: 207.241.237.238
Mozilla 5.0, 
Today: Jan 21, 2013