You are here: Home NEWS Local News U-20 YATINGA ROBO FAINALI, YAICHAPA AYOSSA 5-0

U-20 YATINGA ROBO FAINALI, YAICHAPA AYOSSA 5-0

E-mail Print PDF

VIEWED 700 TIMES

Kikosi cha timu ya vijana wenye umri chini ya miaka 20, U-20 cha Young Africans leo kimekata tiketi ya kucheza Robo Fainal ya mashindano ya El Talento Soccer Tournament Cup 2012 baada ya kuichapa timu ya Ayossa FC mabao 5 - 0 katika mchezo uliofanyika katika Uwanja wa Etihad Stadium - Mwananyamala B.

Vijana wa U-20 wa Young Africans wanashiriki mashindano hayo ambayo mshindi ataibuka na zawadi ya tshs Milioni 3, leo walikuwa wanacheza mchezo wa tatu, kufuatia kushinda 2-1 mchezo wake wa kwanza dhidi ya timu ya Mbagala Market, na sare ya 1-1 dhidi ya Star Rangers

Ayossa FC timu ambayo imemaliza hatua ya makundi pasipo kupata pointi hata moja baada ya kufungwa michezo yote, leo walionekana kukakamia mchezo huo, ukizingatia timu ya U-20 Yanga tangu mwezi wa saba (julai) imeshacheza jumla ya michezo 23, ikishinda michezo 18, sare 4 na kufungwa mchezo mmoja tu dhidi ya timu ya Ruvu Shooting katika mchezo wa utangulizi wa ligi kuu ya Vodacom.

U-20 Yanga waliuanza chezo kwa kasi kwa lengo la kusaka bao la mapema, katika dakika ya 16 kiungo mshambuliaji Rehani Kibingu aliipatia timu ya U-20 bao la kwanza akimalizia kazi nzuri ya George Banda.

Dakika ya 32, Rehani Kibingu tena aliipatia U-20 bao la pili baada ya kuwazidi ujanja walinzi wa Ayossa na kuachia shuti kali lililojaa wavuni moja kwa moja.

Mpira ulikwenda mapumziko, U-20 Yanga 2- 0 Ayossa FC

Kipindi cha pili kilianza kwa kocha mkuu wa U-20 Young Africans kufanya mabadiliko, ya kuwaingiza Notikelly Masasi, Hussein Moshi kuchukua nafasi za Suleiman Ussi na Clever Charles.

Mabdiliko hayo yalileta uhai kwa kikosi cha U-20 kwani dakika ya 46 ya mchezo, mshambuliaji Notikely Masasi aliipatia U-20 bao la tatu kwa njia ya tik tak, akiunganisha krosi safi ya Zuberi Amiri.

Notikely Masasi aliendelea kuwa mwiba kwa walinzi wa Ayossa kwani katika dakika ya 72 ya mchezo aliipatia U-20 bao la nne akimalizia krosi ya Mwinyi Bakari aliywatoka walinzi wa Ayossa na kupiga krosi iliyomkuta mfungaji.

Dakika ya 85, Zuberi Amiri aliipatia U-20 Yanga bao la tano baada ya kupanda kusaidia mashambulizi na kumtoka mlinzi wa Ayossa kisha kumpiga chenga mlinda mlango kabla ya kufunga bao hilo.

Mpaka dakika 90 zinamalizika, U-20 Young Africans 5 - 0 Ayossa FC.

Kwa matokeo hayo U-20 Young Africans imeongeza kundi D kwa kufikisha point 7 baada ya kushinda michezo miwili na kutoka sare mchezo mmoja, hivyo itacheza mchezo wa Robo Fainali siku ya jumatatu saa 1 kasorobo usiku dhidi ya timu ya African People.

Mchezo wa leo ulihudhuriwa na kocha mkuu Ernie Brands aliyekuwa akitazama vipaji vya vijana.

U-20 Yanga: 1.Yusuph Abdallah, 2.Zuberi Amiri, 3.Said Mashaka/Hussein Moshi, 4.Benson Michael, 5.Issa Ngao, 6.Clever Charles 7.Rehani Kibingu, 8.Mwinyi Bakari, 9.George Banda 10.Suleiman Ussi/Notikelly Masasi 11.Abdallah Mnguli

 
  • FACEBOOK PAGE

  • TWITTER FEEDS

yanga1935: Yanga yafanya mkutano mkuu wa wanachama salama, ajenda zote zapitishwa http://t.co/lotRChsL
yanga1935: Yanga yaichapa Black Leopard mabao 3-2 http://t.co/8XbabdSs
yanga1935: Mpira umemalizika, Young Africans 3 - 2 Black Leopard Tegete dkk 32,73, Domayo 63 Khoza dkk 47, Rodney dkk 89
yanga1935: Dakika ya 89, Rodney Ramagalela anaipatia Black Leopard bao la pili kwa mkwaju wa penati
yanga1935: Dakika ya 84, Young Africans inafanya mabadiliko anaingia George Banda anatoka Jerson Tegete
yanga1935: Dakika ya 75, Young Africans 3 - 1 Black Leopard anaingia Said Bahanuzi anatoka Didier Kavumbagu
yanga1935: Dakika ya 73, Jerson Tegete anaipatia Young Africans bao la tatu Young Africans 3 - 1 Black Leopard
yanga1935: Dakika ya 63, Frank Domayo anaipatia Young Africans bao la pili Young Africans 2 - 1 Black Leopard
yanga1935: Dakika ya 60, Young Africans 1 - 1 Black Leopard
yanga1935: Dakika ya 47, Humphrey Khoza anaipatia Black Leopard bao la kusawazisha#Young Africans 1 - 1 Black Leopard
yanga1935: wanaingia Said Mohamed, Saimon Msuva na Juma Abdul Wanatoka Kabange Twite, Mbuyu Twite na Ally Mustafa
yanga1935: Kipindi cha pili cha mchezo kimeanza, Young Africans inafanya mabadiliko wanaingia Said Mohamed, Saimon Msuva na Juma Abdul
yanga1935: Mpira ni mapumziko, Young Africans 1 - 0 Black Leopard Tegete dkk 32
yanga1935: Dakika ya 32, Jerson Tegete anaipatia Young Africans bao la kwanza kwa mkwaju wa penati
yanga1935: Dakika ya 30, Young Africans 0 - 0 Black Leopard
yanga1935: Dakika ya 15, Young Africans 0 - 0 Black Leopard
yanga1935: Mpira ndio umeanza hapa Uwanja wa Taifa kati ya Young Africans Vs Black Leopard
yanga1935: Here's Young Africans line-up to face Black Leopard today#Mustafa,Mbuyu,Oscar,Nadir,Yondani,Chuji,Kabange,Domayo,Didier,Tegete,Niyonzima
yanga1935: International Friendly Match today: #Young Africans Vs Black Leopard Kick-off 16:00hrs Venue: National Stadium
yanga1935: Yanga Vs Black Leopard kesho Taifa http://t.co/o9Uu695M
yanga1935: Yanga yaanza mazoezi baada kurejea kutoka nchini Uturuki http://t.co/WjuE9731
yanga1935: Young Africans kuivaa Black Leopard ya Afrika Kusini http://t.co/O5qJvtLG
yanga1935: Yanga yawasili Dar salama http://t.co/F8W53VAa
mod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_counter
mod_vvisit_counterToday826
mod_vvisit_counterYesterday2888
mod_vvisit_counterThis week826
mod_vvisit_counterLast week17151
mod_vvisit_counterThis month55152
mod_vvisit_counterLast month36036
mod_vvisit_counterAll days293384

We have: 39 guests, 3 bots online
Your IP: 207.241.237.238
Mozilla 5.0, 
Today: Jan 21, 2013