You are here: Home NEWS Local News YANGA UTAIPENDA, YAICHAPA MGAMBO JKT 3-0

YANGA UTAIPENDA, YAICHAPA MGAMBO JKT 3-0

E-mail Print PDF
VIEWED 865 TIMES

Yanga Afrika utaipenda tu, yaichapa 3-0 Mgambo JKT Uwanja wa Taifa na kumkata mnyama, kutoka tofauti ya pointi 10 mpaka tofauti ya bao 1...Yanga kanyaga twende !!!

Safari imeshika kasi kwa mabingwa watetezi wa kombe la Kagame mara mbili mfululizo timu ya Young Africans, leo wameichapa timu ya Mgambo JKT mabao 3-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara, mchezo uliofanyika leo katika Uwanja wa Taifa.

Yanga ambayo imerudisha makali yake katika kinyanganyiro cha Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara, imefikisha jumla ya pointi 23 sawa na Simba SC ambao wanaongoza ligi kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa.
Yanga ilianza mbio za kusaka point 3 muhimu na katika sekunde ya 15 ya mchezo, Mshambuliaji Saimon Msuva alikosa bao la wazi baada ya kupewa pasi nzuri na Haruna Niyonzima, lakini Msuva alishindwa kuukwamisha mpira huo wavuni.

Dakika ya 2 ya mchezo, Nadri Haroub 'Cannavaro' aliipatia Yanga bao la kwanza kwa kichwa, akiunganisha mpira wa faulo uliopigwa na Athuman Idd baada ya mshambuliaji Didier Kavumbagu kuchezewa ndivyo sivyo nje kidogo ya eneo la hatari.
Saimon Msuva, Hamis Kiiza na Haruna Niyonzima walikosa mabao mengi ya wazi katika kipindi cha kwanza kutokana na kutokua makini katika umaliziaji hali iliyopelekea mpaka dakika 30 za mchezo Yanga kuendelea kuwa mbele kwa bao 1 tu.
Didier Kavumbagu aliipatia Yanga bao la pili katika dakika ya 39 baada ya kumalizia pasi nzuri iliyopigwa na mshambuliaji Hamis Kiiza na kumkuta mfungaji ambaye hakufanya ajizi na kuukwamisha mpira huo wavuni na kuhesabu bao lake la tano.
Wachezaji wa timu ya Yanga waliendelea kuutawala mchezo kwa dakika zote za kipindi cha kwanza na kama umaliziaji ungekuwa makini basi Yanga ingeibuka na ushindi mkubwa zaidi katika dakika 45 za kipindi cha kwanza.

Mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza Young Africans 2-0 Mgambo JKT.

Kipindi cha pili kilianza kwa Yanga kufanya mabadiliko kwa kumuingiza Kelvin Yondani aliyekuwa majeruhi kwa mda mrefu kuchukua nafasi ya Shadrack Nsajigwa.
Mabadiliko hayo yalileta uhai kwa vijana wa Jangwani kwani Mbuyu Twite ambaye alirudi kucheza nafasi ya mlinzi wa kulia, alipata nafasi ya kupanda mbele kuongeza nguvu mashambulizi hali iliyopelekea walinzi wa Mgambo JKT kumchezea faulo nyingi sana.
Jeryson Tegete ambaye aliingia kuchukua nafasi ya Didier Kavumbagu aliipatia Yanga bao la tatu baada ya kumalizia krosi safi iliyopigwa na Oscar Joshua aliyepanda kuongeza nguvu mashambulizi na kumkuta Tegete alifunga kwa kupiga shuti kali na mpira kuingia sehemu ya nyavu ndogo za juu.
Kama washambuliaji wa Yanga wangekuwa makini wangeweza kufunga mabao mengi zaidi, lakini kutokua kwao makini katika umaliziaji wa Saimon Msuva, Hamis Kiiza na Haruna Niyonzima uliwafanya wasiweze kupata mabao mengine ya ziada kwani nafasi walizozipata zingeweza kuifanya Yanga iondoke na ushindi mnono.

Mpaka dakika 90 za mchezo za mwamuzi Martin Sanya zinamalizika, Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 3-0 Mgambo JKT

Yanga inajiandaa na mchezo wake dhidi ya Azam Fc siku jumapili, pambano ambalo litafanyika katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Yanga: 1.Ally Mustapha, 2.Shadrack Nsajigwa/Klevin Yondani, 3.Oscar Joshua, 4.Nadir Haroub, 5.Mbuyu Twite, 6.Athuman Idd, 7.Saimon Msuva, 8.Frank Domayo/Nurdin Bakari 9.Didier Kavumbagu/Jeryson Tegete, 10.Hamis Kiiza, 11.Haruna Niyonzima
Last Updated ( Thursday, 01 November 2012 10:39 )  
  • FACEBOOK PAGE

  • TWITTER FEEDS

yanga1935: Yanga yafanya mkutano mkuu wa wanachama salama, ajenda zote zapitishwa http://t.co/lotRChsL
yanga1935: Yanga yaichapa Black Leopard mabao 3-2 http://t.co/8XbabdSs
yanga1935: Mpira umemalizika, Young Africans 3 - 2 Black Leopard Tegete dkk 32,73, Domayo 63 Khoza dkk 47, Rodney dkk 89
yanga1935: Dakika ya 89, Rodney Ramagalela anaipatia Black Leopard bao la pili kwa mkwaju wa penati
yanga1935: Dakika ya 84, Young Africans inafanya mabadiliko anaingia George Banda anatoka Jerson Tegete
yanga1935: Dakika ya 75, Young Africans 3 - 1 Black Leopard anaingia Said Bahanuzi anatoka Didier Kavumbagu
yanga1935: Dakika ya 73, Jerson Tegete anaipatia Young Africans bao la tatu Young Africans 3 - 1 Black Leopard
yanga1935: Dakika ya 63, Frank Domayo anaipatia Young Africans bao la pili Young Africans 2 - 1 Black Leopard
yanga1935: Dakika ya 60, Young Africans 1 - 1 Black Leopard
yanga1935: Dakika ya 47, Humphrey Khoza anaipatia Black Leopard bao la kusawazisha#Young Africans 1 - 1 Black Leopard
yanga1935: wanaingia Said Mohamed, Saimon Msuva na Juma Abdul Wanatoka Kabange Twite, Mbuyu Twite na Ally Mustafa
yanga1935: Kipindi cha pili cha mchezo kimeanza, Young Africans inafanya mabadiliko wanaingia Said Mohamed, Saimon Msuva na Juma Abdul
yanga1935: Mpira ni mapumziko, Young Africans 1 - 0 Black Leopard Tegete dkk 32
yanga1935: Dakika ya 32, Jerson Tegete anaipatia Young Africans bao la kwanza kwa mkwaju wa penati
yanga1935: Dakika ya 30, Young Africans 0 - 0 Black Leopard
yanga1935: Dakika ya 15, Young Africans 0 - 0 Black Leopard
yanga1935: Mpira ndio umeanza hapa Uwanja wa Taifa kati ya Young Africans Vs Black Leopard
yanga1935: Here's Young Africans line-up to face Black Leopard today#Mustafa,Mbuyu,Oscar,Nadir,Yondani,Chuji,Kabange,Domayo,Didier,Tegete,Niyonzima
yanga1935: International Friendly Match today: #Young Africans Vs Black Leopard Kick-off 16:00hrs Venue: National Stadium
yanga1935: Yanga Vs Black Leopard kesho Taifa http://t.co/o9Uu695M
yanga1935: Yanga yaanza mazoezi baada kurejea kutoka nchini Uturuki http://t.co/WjuE9731
yanga1935: Young Africans kuivaa Black Leopard ya Afrika Kusini http://t.co/O5qJvtLG
yanga1935: Yanga yawasili Dar salama http://t.co/F8W53VAa
mod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_counter
mod_vvisit_counterToday693
mod_vvisit_counterYesterday2888
mod_vvisit_counterThis week693
mod_vvisit_counterLast week17151
mod_vvisit_counterThis month55019
mod_vvisit_counterLast month36036
mod_vvisit_counterAll days293251

We have: 35 guests, 1 members, 2 bots online
Your IP: 207.241.237.238
Mozilla 5.0, 
Today: Jan 21, 2013