You are here: Home NEWS Local News YANGA YAWASILI SALAMA ARUSHA, KUIVAA JKT OLJORO KESHO

YANGA YAWASILI SALAMA ARUSHA, KUIVAA JKT OLJORO KESHO

E-mail Print PDF

VIEWED 481 TIMES

Timu ya Young Africans Sports Club kesho jumamosi, itashuka dimbani kucheza dhidi ya timu ya JKT Oljoro FC katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara, mchezo utakaofanyika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.
Kikosi cha wachezaji 20 na benchi la Ufundi 7 kiliwasili salama jana jioni majira ya saa 11, na majira ya saa 12 jioni kilifanya mazoezi mepesi katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid

Young Africans itaingia uwanjani kwa lengo la kusaka pointi 3 muhimu ambazo zinaweza kuipelekea kuongoza Ligi katika msimamo wa Ligi Kuu ya Vodacom endapo mchezo kati ya Simba na Azam ziatatoka sare, na kama Azam au Simba mmoja akishinda na Yanga ikashinda basi itakwea mpaka nafasi ya pili katika msimamo.

Kochaa mkuu wa Yanga mholanzi Ernie Brandts amesema anashukru vijana wake wote vizuri na wamefika salama na hakuna mchezaji majeruhi katika wachezaji waliopo Arusha hivyo anaamini timu yake itaibuka na ushindi.
Katika mchezo wa mwisho dhidi ya Polisi Morogoro Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam , Young Africans iliibuka na ushindi wa mabao 3-0, shukrani kwa mabao ya Saimon Msuva, Didier Kavumbagu na Hamis Kiiza.

Kikosi kitafanya mazoezi katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid leo jioni majira ya 10, yakiwa ni mazoezi ya mwisho kabla ya mpambano hapo kesho.
Wachezaji waliopo Arusha ni:
Walinda Mlango: Yaw Berko, Ally Mustapha 'Barthez'
Walinzi wa Pembeni: Shadrack Nsajigwa, Oscar Joshua, David Luhende,
Walinzi wa Kati: Kelvin Yondani, Mbuyu Twite, Ladisalus Mbogo, Nadir Haroub 'Cannavaro'
Viungo Wakabaji: Frank Domayo, Athuman Idd 'Chuji', Juma Seif 'kijiko'
Viungo Washambuliaji: Haruna Niyonzima, Rashid Gumbo, Nurdin Bakari
Washambuliaji: Saimon Msuva, Nizar Khaflan, Didier Kavumbagu, Hamis Kiiza na Jeryson Tegete
 
  • FACEBOOK PAGE

  • TWITTER FEEDS

yanga1935: Yanga yafanya mkutano mkuu wa wanachama salama, ajenda zote zapitishwa http://t.co/lotRChsL
yanga1935: Yanga yaichapa Black Leopard mabao 3-2 http://t.co/8XbabdSs
yanga1935: Mpira umemalizika, Young Africans 3 - 2 Black Leopard Tegete dkk 32,73, Domayo 63 Khoza dkk 47, Rodney dkk 89
yanga1935: Dakika ya 89, Rodney Ramagalela anaipatia Black Leopard bao la pili kwa mkwaju wa penati
yanga1935: Dakika ya 84, Young Africans inafanya mabadiliko anaingia George Banda anatoka Jerson Tegete
yanga1935: Dakika ya 75, Young Africans 3 - 1 Black Leopard anaingia Said Bahanuzi anatoka Didier Kavumbagu
yanga1935: Dakika ya 73, Jerson Tegete anaipatia Young Africans bao la tatu Young Africans 3 - 1 Black Leopard
yanga1935: Dakika ya 63, Frank Domayo anaipatia Young Africans bao la pili Young Africans 2 - 1 Black Leopard
yanga1935: Dakika ya 60, Young Africans 1 - 1 Black Leopard
yanga1935: Dakika ya 47, Humphrey Khoza anaipatia Black Leopard bao la kusawazisha#Young Africans 1 - 1 Black Leopard
yanga1935: wanaingia Said Mohamed, Saimon Msuva na Juma Abdul Wanatoka Kabange Twite, Mbuyu Twite na Ally Mustafa
yanga1935: Kipindi cha pili cha mchezo kimeanza, Young Africans inafanya mabadiliko wanaingia Said Mohamed, Saimon Msuva na Juma Abdul
yanga1935: Mpira ni mapumziko, Young Africans 1 - 0 Black Leopard Tegete dkk 32
yanga1935: Dakika ya 32, Jerson Tegete anaipatia Young Africans bao la kwanza kwa mkwaju wa penati
yanga1935: Dakika ya 30, Young Africans 0 - 0 Black Leopard
yanga1935: Dakika ya 15, Young Africans 0 - 0 Black Leopard
yanga1935: Mpira ndio umeanza hapa Uwanja wa Taifa kati ya Young Africans Vs Black Leopard
yanga1935: Here's Young Africans line-up to face Black Leopard today#Mustafa,Mbuyu,Oscar,Nadir,Yondani,Chuji,Kabange,Domayo,Didier,Tegete,Niyonzima
yanga1935: International Friendly Match today: #Young Africans Vs Black Leopard Kick-off 16:00hrs Venue: National Stadium
yanga1935: Yanga Vs Black Leopard kesho Taifa http://t.co/o9Uu695M
yanga1935: Yanga yaanza mazoezi baada kurejea kutoka nchini Uturuki http://t.co/WjuE9731
yanga1935: Young Africans kuivaa Black Leopard ya Afrika Kusini http://t.co/O5qJvtLG
yanga1935: Yanga yawasili Dar salama http://t.co/F8W53VAa
mod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_counter
mod_vvisit_counterToday693
mod_vvisit_counterYesterday2888
mod_vvisit_counterThis week693
mod_vvisit_counterLast week17151
mod_vvisit_counterThis month55019
mod_vvisit_counterLast month36036
mod_vvisit_counterAll days293251

We have: 35 guests, 1 members, 2 bots online
Your IP: 207.241.237.238
Mozilla 5.0, 
Today: Jan 21, 2013