You are here: Home NEWS Local News YANGA KUIVAA POLISI MOROGORO TAIFA

YANGA KUIVAA POLISI MOROGORO TAIFA

E-mail Print PDF
VIEWED 630 TIMES
Kocha mkuu wa timu ya Young Africans Sports Club, Mholanzi Ernie Brandts amesema kikosi chake kipo tayari kuikabili timu ya Polisi Morogoro katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom utakaofanyika kesho uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Akiongea na mtandao wa klabu www.youngafricans.co.tz leo asubuhi katika mazoezi yaliyofanyika shule ya sekondari Loyola, amesema wachezaji wake wote wapo safi, wana ari ya mchezo na ushindi, hivyo anaamini mchezaji yoyote atakayempanga atafanya vizuri.

Polisi Morogoro timu iliyoipanda ligi msimu huu 2012/2013 inakamata mkia katika msimamo wa ligi kuu ya Vodacom ikiwa na pointi 2 ilizozipata kwa kutoka sare michezo miwili kati ya michezo saba iliyokwishacheza.
Yanga ambayo mchezo wake wa mwisho iliibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya timu ya Ruvu Shooting katika mchezo uliochezwa mwishoni mwa wiki, itaingia uwanjani kusaka pointi 3 muhimu zitakazo isogeza mpaka nafasi tatu za juu na kupunguza tofauti ya point na mtani wake wa jadi Simba anayeongoza ligi kwa pointi 19.
Katika mazoezi yaliyofanyika leo asubuhi, kocha Brandts ameendelea kufurahia kuwepo kwa wachezaji wake wote, kitu kitakachopelea kumtumia mchezaji yoyote atakayetaka kumtumia kwa mchezo huo wa kesho, kwani hakuna mchezaji aliye majeruhi .
Vijana wa jangwani kwa sasa wanakamata nafasi ya tatu katika msimao wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara kwa kufikisha point 14 nyuma ya Azam yenye pointi 17 na Simba yenye pointi 19 ikiwa mbele kwa mchezo mmoja.

Mchezo utaanza majira ya saa 10:30 jioni kwa saa za Afrika Mashariki na viingilio vya mchezo huo ni:
VIP A 20,000/=
VIP B &C; 15,000/=
Orange 8,000/=
Blue & Green 5,000/=

'MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI YOUNG AFRICANS'

'DAIMA MBELE NYUMA MWIKO'
Last Updated ( Tuesday, 23 October 2012 09:54 )  
  • FACEBOOK PAGE

  • TWITTER FEEDS

yanga1935: Yanga yafanya mkutano mkuu wa wanachama salama, ajenda zote zapitishwa http://t.co/lotRChsL
yanga1935: Yanga yaichapa Black Leopard mabao 3-2 http://t.co/8XbabdSs
yanga1935: Mpira umemalizika, Young Africans 3 - 2 Black Leopard Tegete dkk 32,73, Domayo 63 Khoza dkk 47, Rodney dkk 89
yanga1935: Dakika ya 89, Rodney Ramagalela anaipatia Black Leopard bao la pili kwa mkwaju wa penati
yanga1935: Dakika ya 84, Young Africans inafanya mabadiliko anaingia George Banda anatoka Jerson Tegete
yanga1935: Dakika ya 75, Young Africans 3 - 1 Black Leopard anaingia Said Bahanuzi anatoka Didier Kavumbagu
yanga1935: Dakika ya 73, Jerson Tegete anaipatia Young Africans bao la tatu Young Africans 3 - 1 Black Leopard
yanga1935: Dakika ya 63, Frank Domayo anaipatia Young Africans bao la pili Young Africans 2 - 1 Black Leopard
yanga1935: Dakika ya 60, Young Africans 1 - 1 Black Leopard
yanga1935: Dakika ya 47, Humphrey Khoza anaipatia Black Leopard bao la kusawazisha#Young Africans 1 - 1 Black Leopard
yanga1935: wanaingia Said Mohamed, Saimon Msuva na Juma Abdul Wanatoka Kabange Twite, Mbuyu Twite na Ally Mustafa
yanga1935: Kipindi cha pili cha mchezo kimeanza, Young Africans inafanya mabadiliko wanaingia Said Mohamed, Saimon Msuva na Juma Abdul
yanga1935: Mpira ni mapumziko, Young Africans 1 - 0 Black Leopard Tegete dkk 32
yanga1935: Dakika ya 32, Jerson Tegete anaipatia Young Africans bao la kwanza kwa mkwaju wa penati
yanga1935: Dakika ya 30, Young Africans 0 - 0 Black Leopard
yanga1935: Dakika ya 15, Young Africans 0 - 0 Black Leopard
yanga1935: Mpira ndio umeanza hapa Uwanja wa Taifa kati ya Young Africans Vs Black Leopard
yanga1935: Here's Young Africans line-up to face Black Leopard today#Mustafa,Mbuyu,Oscar,Nadir,Yondani,Chuji,Kabange,Domayo,Didier,Tegete,Niyonzima
yanga1935: International Friendly Match today: #Young Africans Vs Black Leopard Kick-off 16:00hrs Venue: National Stadium
yanga1935: Yanga Vs Black Leopard kesho Taifa http://t.co/o9Uu695M
yanga1935: Yanga yaanza mazoezi baada kurejea kutoka nchini Uturuki http://t.co/WjuE9731
yanga1935: Young Africans kuivaa Black Leopard ya Afrika Kusini http://t.co/O5qJvtLG
yanga1935: Yanga yawasili Dar salama http://t.co/F8W53VAa
mod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_counter
mod_vvisit_counterToday693
mod_vvisit_counterYesterday2888
mod_vvisit_counterThis week693
mod_vvisit_counterLast week17151
mod_vvisit_counterThis month55019
mod_vvisit_counterLast month36036
mod_vvisit_counterAll days293251

We have: 34 guests, 1 members, 2 bots online
Your IP: 207.241.237.238
Mozilla 5.0, 
Today: Jan 21, 2013