You are here: Home NEWS Local News MBUYU TWITE ATUA RASMI YANGA

MBUYU TWITE ATUA RASMI YANGA

E-mail Print PDF

2012-08-12 12:44:57 VIEWED 2250 TIMES

Mlinzi wa kati wa timu ya APR kutoka nchini Rwanda Mbuyu Twite amekamilisha usajili wake ikiwa ni pamoja na kupata uhamisho wa kimataifa ITC na kuweza kujiunga na mabingwa wa kombe la klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati kombe la Kagame timu ya Young Africans Sports Club.

 

 

 

 

 

 

Mbuyu Twite amabye zoezi lake la usajili lilianza takribani wiki mbili zilizopita limefikia mwisho baada ya klabu ya Young Africans kufanikiwa kupata uhamisho wake wa kimataifa kutoka timu aliyokuwa akiichezea ya APR ambapo awali alikuwa akiichezea timu ya st. Lumpopo FC

Twite ambaye alingara sana katika mashindano ya Kagame yaliyomalizika hivi karibuni na Young Africans kuibuka mabingwa, amesema anajisikia furaha na mwenye bahati kufanikiwa kujiunga na mabingwa mara mbili mfululizo wa kombe la Kagame.

Usajili wa Twite ulianza takribani wiki mbili zilizopita ambapo mjumbe wa kamati ya Utendaji wa klabu ya Young Africans Abdallah Bin Kleb aliamua kwenda nchini Rwanda kuhakiksiha zoezi hilo linakamilika haraka ipasavyo, ambapo mara baada ya kumalizana na Twite aliendelea kuhakikisha anafuatilia ITC yake nchini DRC.

Akiongea na www.youngafricans.co.tz Bin Kleb amesema, Young Africans ni timu kubwa katika Ukanda huu, Viongozi wake wanafanya mambo yao kwa uhakika zaidi, hivyo hawakutaka kuongelea suala la Twite mpaka watakapoona wamekamilisha zoezi lote'

"Unajua usajili sio mchezaji kusaini makaratasi ya mkataba tu, kuna kupata barua ya kumruhusu kutoka timu anayotoka, uhamisho wa mchezaji kutoka chama husika cha soka cha nchi, baada ya hapo ndio unaweza kutangaza sasa kwamba ni mchezaji wako halali"alisema Bin Kleb.

Kusajiliwa kwa Mbuyu Twite kunaifanya timu ya Young Africans kuwa na ukuta wa walinzi wa kimataifa akiwemo Kelvin Yondani, Nadir Haroub Cannavaro, Ladislau Mbogo na Ibrahim Job kwa nafasi ya ulinzi wa katikati.

Twite anatarajiwa kuwasili mapema wikii kuungana na wacheji wenzake katika mazoezi ya maandalizi ya msimu mpya wa ligi kuu Tanzania bara inayotarajiwa kuaanza sepetemba mosi.

 

Last Updated ( Sunday, 12 August 2012 10:31 )  

OUR SPONSORS

  • FACEBOOK PAGE

  • TWITTER FEEDS

yanga1935: YANGA YAWASILISHA USAJILI TFF http://t.co/tVQKjNaS
yanga1935: MBUYU TWITE ATUA RASMI YANGA http://t.co/cHvnG4ox
yanga1935: YANGA YAENDELEA KUJIFUA http://t.co/lLW7QKE4
yanga1935: Sintah - Dar es Salaam, Tanzania http://t.co/Wb31LLFl
mod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_counter
mod_vvisit_counterToday99
mod_vvisit_counterYesterday1346
mod_vvisit_counterThis week5218
mod_vvisit_counterLast week9772
mod_vvisit_counterThis month22162
mod_vvisit_counterLast month27959
mod_vvisit_counterAll days95913

We have: 8 guests, 2 bots online
Your IP: 204.236.235.245
 , 
Today: Aug 17, 2012