You are here: Home NEWS Local News

Local News

News

YANGA YAREJEA DAR, KUIVAA MGAMBO JUMAMOSI

VIEWED 2591 TIMES

Kikosi cha timu ya Young Africans tayari kimesharejea jijini Dar es salaam kutok kanda ya Ziwa ambapo kilicheza michezo miwili ya Ligi Kuu ya Vodacom dhidi ya Stand United ya mjini Shinyanga na Kagera Sugar ya mjini Bukoba na kujikusanyia pointi tatu kati ya pointi sita.

Last Updated on Tuesday, 04 November 2014 09:06

Read more...

 

News

YANGA KUIVAA KAGERA KESHO

VIEWED 2313 TIMES

Kikosi cha timu ya Young Africans kesho (jumamosi) kitashuka dimbani kusaka pointi tatu muhimu kutoka kwa wenyeji timu ya wakata miwa Kagera Sugar mchezo utakaochezwa kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.

Last Updated on Friday, 31 October 2014 12:09

Read more...

 

News

YANGA YAJIFUA KAHAMA, KUCHEZA NA AMBASSADOR JUMATANO

VIEWED 2719 TIMES

Kikosi cha Young Africans kimewasili jana mjini Kahama ambapo kitaweka kambi ya siku ya tatu kabla ya kuelekea mjini Bukoba kwa ajili ya mchezo wake wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara siku ya jumamosi dhidi ya wenyeji timu ya Kagera Sugar.

Last Updated on Monday, 27 October 2014 09:05

Read more...

   

News

YANGA YAICHAPA STAND UTD 3-0

Young Africans imewachapa wenyeji timu ya Stand United kwa mabao 3-0, katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom uliofanyika jioni ya leo katika Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga, huku mshambulaji Jerson Tegete akibuka mchezaji bora wa mchezo kwa kukwaisha wavuni mabao mawili peke yake.

Kocha Marcio Maximo leo alibadilisha mfumo kwa Haruna Niyonzima kucheza zaidi pembeni, na kiungo Andrey Coutinho kucheza dimba la juu hali iliyopelekea timu kufanya mashambulizi mengi langoni mwa timu ya Stand United,

Dakika ya 12 ya mchezo, mshambuliaji raia wa Brazil Geilson Santana "Jaja" aliwainua vitini mashabiki waliojitokeza uwanjani kwa kuipatia timu yake bao la kwanza akimalizia pasi nzuri ya kiungo Andrey Coutinho.

Mara baada ya bao hilo wenyeji Stand walicharuka na kusaka bao la kusawazisha lakini umakini wa walinzi wa Yanga walikua kikwazo kwao, na kujikuta wakishambulia bila mafanikio.

Mpaka dakika 45 za kipindi cha pili cha kwanza zinamalizika, Young Africans ilikuwa mbele kwa bao 1- 0.

Kipindi cha pili cha mchezo kilianza kwa Young Africans kufanya mabadiliko ambapo waliingia Hussein Javu na Jerson Tegete kuchukua nafasi za Andrey Coutinho na Geilson Santana "Jaja" mabadiliko yaliyosaidia na kubadilisha hali ya mchezo.

Dakika ya 78 ya mchezo, mshambuliaji Jerson Tegete aliipatia Young Africans bao la pili la mchezo kwa kumchambua mlianda mlango wa Stand United baada ya kupenyezewa pasi safi na Hussein Javu.

Huku watu wakiwa wameanza kutoka Uwanjani wakifiri mchezo umemalizika, Jerson Tegete tena aliipatia Young Africans bao la tatu na la ushindi baada ya kupokea pasi ya Hassan Dilunga aliyewatoka walinzi wa Stand United na kuukwamisha mpira wavuni.

Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika, Young Africans 3 - 0 Stand United.

Mara baada ya mchezo huo, kocha mkuu wa Young Africans Marcio Maximo aliwapongeza wachezaji wake kwa kazi nzuri waliofanya na kusema maandalizi dhidi ya Kagera Suagr yanaanza mara moja.

Young Africans: 1.Deo Munish "Dida", 2. Juma Abdul, 3. Oscar Joshua, 4. Nadir Haroub "Cannavaro", 5.Kelvin Yondani, 6. Mbuyu Twite, 7. Hassan Dilunga, 8. Coutinho, 9. Jaja/Tegete, 10.Mrisho Ngasa, 11.Haruna Niyonzima/Nizar

 

News

YANGA YAICHAPA STAND UTD 3-0

VIEWED 4151 TIMES

Young Africans imewachapa wenyeji timu ya Stand United kwa mabao 3-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom uliofanyika jioni ya leo katika Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga, huku mshambulaji Jerson Tegete akibuka mchezaji bora wa mchezo kwa kukwamisha wavuni mabao mawili peke yake.

Last Updated on Sunday, 26 October 2014 00:23

Read more...

   

  • FACEBOOK

  • TWITTER